PATA HABARI MOTO MOTO, ZA KITAIFA NA KIMATAIFA KUPITIA HAPA, TUPE MAWAZO YAKO TUYAFANYIE KAZI, TUPE HABARI ZOZOTE ULIZO NAZO TUTAZIWEKA HAPA,KWA MWENYE PARTY AINA YOYOTE INAYOHUSIANA NA MAMBO YA MUSIC, TAFADHARI ONGEA NA PAPAYA KUPITIA NAMBA HII..07501 202029..YUPO MACHO 24/7 BEI MAELEWANO.

Tuesday, 24 January 2012

MATONYA KUMILIKI HOTEL SOON, BONGO FLAVA OYEE!!!



UKIANGALIA historia yake, hakika unaweza kusema amefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kampeni za kuuaga umasikini.

Cha kufurahisha zaidi ni kwamba, ameyapata mafanikio hayo kupitia muziki wa kizazi kipya ambao katika miaka ya hivi karibuni umekuwa na mvuto, na pia ni `biashara’ kubwa kwa wanaoweza kuzichanga vyema karata zao.

Tunamzungumzia Seif Shaaban, maarufu kama Matonya ambaye baada ya muongo mmoja wa kupigana kisanii, sasa anaanza kula matunda ya kipaji chake. Leo hii, Matonya wa kwenye muziki ni `milionea’ fulani hivi.

Na umilionea wake hakuurithi, bali ameusotea, akadunduliza na sasa ana jeuri ya kuitwa Mkurugenzi. Anamiliki biashara kadhaa, ikiwamo ya kuuza magari, lakini sasa amekuja na kitu kipya, hoteli yenye hadhi ambayo iko mbioni kuzinduliwa, baada ya kumtafuna msanii huyo zaidi ya Sh milioni 150.

Katika mazungumzo na gazeti hili hivi karibuni, Matonya amethibitisha kuwa ndiye mmiliki wa hoteli hiyo iliyopo katikati ya Jiji la Tanga.

“Ni hoteli yangu, mali yangu iliyotokana na jasho la kazi yangu,” anasema mkali huyo ambaye aliwahi kuzushiwa kufanya biashara ya dawa za kulevya na kukamatwa China, uzushi alioukana na kusema “sifanyi biashara hiyo, sifikirii kuifanya na wala sijawahi kukanyaga China”.

Anasisitiza kuwa, mafanikio yake yanatokana na kukuna kichwa na kutoa tungo na mashairi yenye hisia kali na mvuto kwa mashabiki wake, ndiyo maana ameweza kufanikiwa. “Tangu nianze muziki kazi zangu zimekuwa zikikubalika, nikaongeza idadi ya mashabiki wa ndani na nje ya nchi.

“Ndiyo maana kila kukicha nimekuwa nikipata mialiko ya kutumbuiza sehemu mbalimbali duniani, Ulaya, Marekani na hata Afrika nimezunguka,” anasema na kuhoji katika mazingira ya aina hiyo, kwa nini abaki katika maisha yale yale ya U-Matonya?

Anaongeza kusema: “Ndiyo maana mpaka hoteli yangu inafikia hatua hii, kila pesa imetoka mfukoni mwangu. Hata benki sijapiga hodi kukopa pesa ya biashara yangu hii ambayo natarajia kuizindua wakati wowote kuanzia sasa.”

Na wakati anajipanga kuizindua hoteli hiyo ambayo anaitafutia jina, Matonya yuko katika hatua za mwisho za kutoa kazi yake mpya kisanii, wimbo aliodai utakuwa gumzo unaoitwa Lesbian, yaani `Usagaji’. Katika wimbo huo, amewashirikisha wakali Abdul Naseeb `Diamond’ na Albert Mangweha `Ngwair’.

Kama ilivyo katika nyimbo zake zilizotangulia, nao umeangukia katika `mahaba’. Tofauti na mawazo ya wengi kuwa wasanii wanapaswa kubadilisha mwelekeo na kuachana na nyimbo za mapenzi, Matonya anasema nyimbo za mapenzi ndizo zinazouza.

“Kuna nyimbo nyingi za kusifia nchi, lakini hazifanyi vizuri sokoni ila nyimbo za mapenzi ndiyo zinauza,” anasema kijana huyo wa Kisambaa aliyekulia Barabara ya Tatu mjini Tanga. Miongoni mwa nyimbo za mapenzi zilizompatia umaarufu mkubwa Matonya ni pamoja na Anitha, Violeth, Taxi Bubu na nyingine kadha wa kadha.

Lakini kwa nini anaitwa Matonya? Mwenyewe anajibu: “Kweli kabisa nilikuwa napiga sana `mizinga’ marafiki zangu wakati nataka kurekodi kibao cha Uaminifu mwaka 2000, ndiyo maana wakaamua kunipa jina hilo nami nikalipokea.

Ndiyo, nilishajipanga kimuziki, lakini sikuwa na pesa za kuingia studio kurekodi, sikuona aibu kusaka pesa ya studio.” Anafafanua kuwa, wakati huo alikuwa kidato cha nne Sekondari ya Sahare iliyopo mjini Tanga.

Majibu yake yanatoa majibu mengine, ya kisa cha yeye kuitwa Matonya, jina la ombaomba maarufu nchini ambaye jina lake halisi ni Paulo Mawezi. Mzee huyo alipata umaarufu mkubwa baada ya `kusumbuana’ sana na aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Yusuf Makamba ambaye licha ya kumtimua mara kadhaa katika jiji hilo.

Staili yake ya kuomba kwa kawaida huwa ni `burudani’. Hulala chali huku mkono akiwa ameunyoosha juu kwa muda mrefu bila ya kutikisika hata kama jua ni kali kupita kiasi.

Huyo ndiye Matonya wa kwenye muziki ambaye baada ya kusota kwa miaka kadhaa, hatimaye ameanza kufungua milango ya mafanikio na sasa anatumia kila anachokipata kwa ajili ya ustawi wa maisha yake na familia yake na mkewe Miriam aliyezaa naye mtoto mmoja, Imran.

Je, atafanikiwa zaidi kibiashara? Bila shaka, kama ameweza kufika hapo, huenda akazidi kupaa na hivyo kutoa funzo kwa wasanii wengine nchini kuwa, kuna maisha mengine nje ya jukwaa la muziki.Cha kufurahisha zaidi ni kwamba, ameyapata mafanikio hayo kupitia muziki wa kizazi kipya ambao katika miaka ya hivi karibuni umekuwa na mvuto, na pia ni `biashara’ kubwa kwa wanaoweza kuzichanga vyema karata zao.

Tunamzungumzia Seif Shaaban, maarufu kama Matonya ambaye baada ya muongo mmoja wa kupigana kisanii, sasa anaanza kula matunda ya kipaji chake. Leo hii, Matonya wa kwenye muziki ni `milionea’ fulani hivi.

Na umilionea wake hakuurithi, bali ameusotea, akadunduliza na sasa ana jeuri ya kuitwa Mkurugenzi. Anamiliki biashara kadhaa, ikiwamo ya kuuza magari, lakini sasa amekuja na kitu kipya, hoteli yenye hadhi ambayo iko mbioni kuzinduliwa, baada ya kumtafuna msanii huyo zaidi ya Sh milioni 150.

Katika mazungumzo na gazeti hili hivi karibuni, Matonya amethibitisha kuwa ndiye mmiliki wa hoteli hiyo iliyopo katikati ya Jiji la Tanga.

“Ni hoteli yangu, mali yangu iliyotokana na jasho la kazi yangu,” anasema mkali huyo ambaye aliwahi kuzushiwa kufanya biashara ya dawa za kulevya na kukamatwa China, uzushi alioukana na kusema “sifanyi biashara hiyo, sifikirii kuifanya na wala sijawahi kukanyaga China”.

Anasisitiza kuwa, mafanikio yake yanatokana na kukuna kichwa na kutoa tungo na mashairi yenye hisia kali na mvuto kwa mashabiki wake, ndiyo maana ameweza kufanikiwa. “Tangu nianze muziki kazi zangu zimekuwa zikikubalika, nikaongeza idadi ya mashabiki wa ndani na nje ya nchi.

“Ndiyo maana kila kukicha nimekuwa nikipata mialiko ya kutumbuiza sehemu mbalimbali duniani, Ulaya, Marekani na hata Afrika nimezunguka,” anasema na kuhoji katika mazingira ya aina hiyo, kwa nini abaki katika maisha yale yale ya U-Matonya?

Anaongeza kusema: “Ndiyo maana mpaka hoteli yangu inafikia hatua hii, kila pesa imetoka mfukoni mwangu. Hata benki sijapiga hodi kukopa pesa ya biashara yangu hii ambayo natarajia kuizindua wakati wowote kuanzia sasa.”

Na wakati anajipanga kuizindua hoteli hiyo ambayo anaitafutia jina, Matonya yuko katika hatua za mwisho za kutoa kazi yake mpya kisanii, wimbo aliodai utakuwa gumzo unaoitwa Lesbian, yaani `Usagaji’. Katika wimbo huo, amewashirikisha wakali Abdul Naseeb `Diamond’ na Albert Mangweha `Ngwair’.

Kama ilivyo katika nyimbo zake zilizotangulia, nao umeangukia katika `mahaba’. Tofauti na mawazo ya wengi kuwa wasanii wanapaswa kubadilisha mwelekeo na kuachana na nyimbo za mapenzi, Matonya anasema nyimbo za mapenzi ndizo zinazouza.

“Kuna nyimbo nyingi za kusifia nchi, lakini hazifanyi vizuri sokoni ila nyimbo za mapenzi ndiyo zinauza,” anasema kijana huyo wa Kisambaa aliyekulia Barabara ya Tatu mjini Tanga. Miongoni mwa nyimbo za mapenzi zilizompatia umaarufu mkubwa Matonya ni pamoja na Anitha, Violeth, Taxi Bubu na nyingine kadha wa kadha.

Lakini kwa nini anaitwa Matonya? Mwenyewe anajibu: “Kweli kabisa nilikuwa napiga sana `mizinga’ marafiki zangu wakati nataka kurekodi kibao cha Uaminifu mwaka 2000, ndiyo maana wakaamua kunipa jina hilo nami nikalipokea.

Ndiyo, nilishajipanga kimuziki, lakini sikuwa na pesa za kuingia studio kurekodi, sikuona aibu kusaka pesa ya studio.” Anafafanua kuwa, wakati huo alikuwa kidato cha nne Sekondari ya Sahare iliyopo mjini Tanga.

Majibu yake yanatoa majibu mengine, ya kisa cha yeye kuitwa Matonya, jina la ombaomba maarufu nchini ambaye jina lake halisi ni Paulo Mawezi. Mzee huyo alipata umaarufu mkubwa baada ya `kusumbuana’ sana na aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Yusuf Makamba ambaye licha ya kumtimua mara kadhaa katika jiji hilo.

Staili yake ya kuomba kwa kawaida huwa ni `burudani’. Hulala chali huku mkono akiwa ameunyoosha juu kwa muda mrefu bila ya kutikisika hata kama jua ni kali kupita kiasi.

Huyo ndiye Matonya wa kwenye muziki ambaye baada ya kusota kwa miaka kadhaa, hatimaye ameanza kufungua milango ya mafanikio na sasa anatumia kila anachokipata kwa ajili ya ustawi wa maisha yake na familia yake na mkewe Miriam aliyezaa naye mtoto mmoja, Imran.

Je, atafanikiwa zaidi kibiashara? Bila shaka, kama ameweza kufika hapo, huenda akazidi kupaa na hivyo kutoa funzo kwa wasanii wengine nchini kuwa, kuna maisha mengine nje ya jukwaa la muziki.

Saturday, 21 January 2012

CHEKENI MNENEPE, WADAU


Mwizi na Mlegezo

Saggy
Mtindo wa Kata K
Mwizi mmoja hapa London aliyekuwa akijaribu kukimbia baada ya kufanya wizi wake, aliuhisi mkono wa sheria ukimkamata baada ya kuanguka, kwa kuwa alikuwa amevaa suruali yake katika mtindo uitwao mlegezo, au kata K.
Gazeti la Metro limesema John O'Dell alisimamishwa na polisi katika eneo la harringey, kaskazini mwa London siku ya Jumapili, lakini badala yake akaamua kukimbia.
Hata hivyo, kwa kuwa alikuwa amevaa suruali yake bila mkanda na katika mtindo wa mlegezo, suruali hiyo iliteremka na kumfanya adondoke na kukamatwa na polisi mara moja. Tukio hilo lilishuhudiwa na wapita njia. Mpita njia Harry Robbins aliyeshuhudia sakata hilo amesema, kwa kuwa hakuwa amevaa mkanda, ilikuwa ni kichekesho jinsi suruali yake mwenyewe ilivyomuangusha na kusababisha kukamatwa. Wote tuliokuwepo tulibaki tukicheka, amesema Robbins. Mwizi huyo baada ya kukamatwa alikiri kuiba laptop ya karibu dola mia tano -- atafikishwa mahakamani Januari 31.

Mimba ya Mochuari

Mochuari
Mfanyakazi wa mochuari

Mwanamama mmoja nchini Marekani anayefanya kazi mochuari ameingia matatani baada ya kupata uja uzito kwa kujamiiana na mtu aliyekufa. Mtandao wa habari wa dead serious news umesema tukio hilo linadhaniwa kutokea katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Mourning Glory, nje ya Lexington, Missouri.
Polisi wa mjini humo wamemshtaki mama huyo aitwaye Felicity Marmaduke kwa kosa la kunajisi na kuchezea maiti. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na polisi, kiungo cha kiume cha mwili wa mtu aliyekufa kilihamasika wakati mwili ukioshwa. Taarifa zinasema, kwa kuwa mwanamama huyo alikuwa peke yake, aliamua kujamiiana na mwili huo.
Kwa mshangao hata wa mwanamama huyo, maiti huyo alitoa mbegu za kiume. Wiki chache baadaye Bi Marmaduke alijikuta ni mja mzito. Baada ya kumwambia daktari wake mfululizo wa matukio, daktari huyo aliwataarifu polisi.
Bi Marmaduke alikamatwa na polisi akiwa nyumabni kwake, si mbali sana na mochuari anayofanyia kazi. Katika tukio la kushangaza zaidi, mwanamama huyo amesema anapanga kudai urithi kutoka kwa familia ya mtu huyo aliyekufa.

Wasiolia kupewa adhabu?

Kim
Mazishi ya Kim Jong-il
Mamlaka za Korea kaskazini zinadaiwa kuwaadhibu wananchi wake kwa kuwapeleka jela na kazi ngumu-- wale wote ambao hawakulia vya kutosha katika msiba wa kiongozi wao Kim Jong-il.
Gazeti la kila siku lenye makao yake makuu Korea Kusini NK limesema yeyote ambaye hakushiriki misa ya kihistoria ya kumuenzi Kim au ambaye alihudhuria lakini hakulia kiasi cha kutosha au kuonekana kulia kwa uongo, atapelekwa katika kambi maalum na kufanyishwa kazi ngumu kwa miezi sita, limeripoti gazeti hilo.
Gazeti hilo limedai huku likikariri chanzo ambacho haikukitaja kuwa yeyote aliyejaribu kutoka nje ya nchi wakati huo atashtakiwa katika mahakama mbele ya kadamnasi. Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa kwenye mtandao wa cnews.com, wengine watapelekwa katika kambi na kupewa elimu upya ya utaifa.
Hakuna taarifa rasmi kutoka Korea kaskazini iliyothibitisha taarifa hizi. Hata hivyo shirika la habari la Korea Kaskazini limeripoti wiki iliyopita kuwa kifo cha Kim Jong-il kiliombolezwa hadi na wanyama wa porini.
"Dubu mmoja akiwa na wanae walionekana wakiwa wanalia kwa nguvu" imesema taarifa ya shirika hilo. Madubu hao sio wanyama pekee ambao wameripotiwa kumuomboleza kiongozi huyo.
Shirika hilo liliripoti mwezi uliopita kuwa mamia ya kunguru aina ya Magpies walionekana wakipeperuka kuzunguka sanamu la Rais Kim katika wilaya ya Magyondae.

Polisi mwizi

Police
Polisi wa Moscow

Polisi katika mji wa St Petersburg wamesema wamemkamata afisa wa polisi akiwa anaendesha gari la wizi.
Gazeti la RIA Novosti limeripoti siku ya Alhamis kuwa polisi huyo kapteni Andrei Makononeko alikutwa akiendesha gari ya wizi aina ya Lexus na huenda akafunguliwa mashtaka. Kamati ya uchunguzi ya Urusi imesema polisi huyo alikamatwa Januari 10. Gari hilo liliibiwa mwezi Novemba, wamesema polisi. Uchunguzi unafanyika kutazama iwapo mashtaka yafunguliwe dhidi ya afisa huyo.

Usipige 999 hovyo

Police
Polisi wa Uingereza
Polisi wa Uingereza wamewataka wananchi wake kutotumia hovyo namba ya dharura, baada ya mtu mmoja kupiga simu na kuripoti ugomvi uliokuwa ukitokea kwenye TV.
Mtandao wa MSN umesema bwana mmoja alipiga simu polisi baada ya ugomvi kuzuka katika tamthilia aliyokuwa akitazama kwenye TV.
Taarifa zinasema bwana huyo alikuwa akitazama tamthilia maarufu Uingereza iitwayo EastEanders, na kipande hicho chenye mzozano kilirekodiwa mwaka 2009. Taarifa za polisi zimetolewa ili kuwafahamisha wananchi umuhimu wa kutumia simuza dharura, na kuainisha zipi ni dharura na zipi sio dharura.

WANAWAKE WAPIGWA KWA KUVAA SURUALI, MALAWI



 20 Januari, 2012 - Saa 13:07 GMT
Rais Bingu wa Mutharika
Takriban watu 3,000 wamekusanyika Blantyre nchini Malawi kupinga mashambulio dhidi ya wanawake wanaovaa suruali.
Baadhi ya wachuuzi wa kike wiki hii walipigwa na kuvuliwa nguo kwenye mitaa ya mji mkuu, Lilongwe, na Blantyre kwa kutovaa mavazi ya asili.
Mmoja aliyeandaa maandamano hayo ameiambia BBC amewasihi wanawake kujitokeza wakiwa wamevaa suruali na fulana nyeupe kuonyesha kukasirishwa kwao.
Rais Bingu wa Mutharika alisema kupitia redio ya taifa kuwa wanawake wana haki ya kuvaa wanachotaka.
Alikana taarifa kuwa aliamuru wanawake waache kuvaa suruali.
Mpaka mwaka 1994, wanawake kwenye nchi hiyo ya kusini mwa Afrika yenye misimamo mikali walikatazwa kuvaa suruali au sketi fupi chini ya uongozi wa kidikiteta wa Hastings Banda.
Wanaume pia walikatazwa kuwa na nywele ndefu.
Wanawake pia wameshambuliwa kwa kuvaa suruali katika nchi za Kenya, Afrika Kusini na Zimbabwe katika miaka ya hivi karibuni.

'Kukatishwa tamaa kutokana na hali ya uchumi'

Mwandishi wa BBC aliyopo Blantyre Raphael Tenthani alisema makamu wa Rais Joyce Banda, waziri wa jinsia, wabunge kadhaa, wahadhiri wa chuo kikuu na wanaharakati walihudhuria maandamano ya Ijumaa.
Seodi White, mwanasheria na mwanaharakati wa haki za wanawake na aliyeandaa maandamano hayo, alisema wanawake hao hawakuvaa mavazi yasiyo ya heshima.
"Ndio Malawi ni nchi yenye msimamo mkali. Lakini tumekuwa tukivaa tunavyotaka, kwa kiwango cha heshima inayotakiwa, ambayo ni kiwango cha watu wote duniani, kwa miaka 18. Na hakuna anayeweza kusimama akasema ni kinyume na Wamalawi, " alikiambia kipindi cha Network Afrika cha BBC.
Alisema wanawake walikuwa wakilengwa na vijana ambao hawafurahishwi na hali ya kiuchumi nchini humo.
"Wachuuzi unaowaona mitaani si watu wazima. Hawa ni vijana, wadogo wa kuwa hata umri wa watoto wangu.
"Wananieleza mimi kuhusu utamaduni? Wananiambia mimi namna ya kuvaa?
"Hivi hili suala kweli ni kuhusu utamaduni au kitu kingine kinachohusiana na hali ngumu ya uchumi wanayokubaliana nayo watu wakitafuta namna ya kutoa hasira zao?
Awali, Bi Banda pia alilaumu mashambulio hayo kutokea kutokana na uchumi nchini Malawi, ambapo kwa sasa kuna upungufu mkubwa wa mafuta na fedha za kigeni.