PATA HABARI MOTO MOTO, ZA KITAIFA NA KIMATAIFA KUPITIA HAPA, TUPE MAWAZO YAKO TUYAFANYIE KAZI, TUPE HABARI ZOZOTE ULIZO NAZO TUTAZIWEKA HAPA,KWA MWENYE PARTY AINA YOYOTE INAYOHUSIANA NA MAMBO YA MUSIC, TAFADHARI ONGEA NA PAPAYA KUPITIA NAMBA HII..07501 202029..YUPO MACHO 24/7 BEI MAELEWANO.

Tuesday, 10 January 2012

RAIS WA GUINEA-BISSAU AFARIKI DUNIA!!

Rais wa Guinea-Bissau Malam Bacai Sanha amefariki dunia hospitalini mjini Paris, imeripoti redio ya taifa.
Rais huyo mwenye umri wa miaka 64, aliyepata urais mwaka 2009, alisafiri kwenda Ufaransa kwa ajili ya kupata matibabu mwishoni mwa Novemba baada ya kupelekwa akiwa mahututi.
Maradhi yaliyokuwa yakimkabili hayajaelezwa hadharani lakini ilikuwa ikijulikana kuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari.
Bw Sanha awali alikuwa akitibiwa katika chumba cha wagonjwa mahututi kwenye hospitali ya nchi jirani ya Senegal.
Amefariki dunia kwenye hospitali ya kijeshi ya Val de Grace kwenye mji mkuu wa Ufaransa.
Rais huyo amekuwa akilazwa mara kwa mara nje ya nchi tangu awe kiongozi wa Guinea-Bissau.
Aliyemtangulia rais, Joao Bernardo Vieira, aliuliwa na askari walioasi.
Nchi hiyo imejikuta kwenye mapinduzi ya mara kwa mara na ghasia tangu kupata uhuru kutoka kwa Wareno mwaka 1974, na imekuwa eneo la kufanya biashara ya dawa za kulevya baina ya Amerika ya kusini na Ulaya.
Mwishoni wa Desemba mkuu wa jeshi la majini, Jose Americo Bubo Na Tchuto, alikamatwa na kutuhumiwa kwa kutaka kuchukua madaraka bila ya kuwepo kwa Bw Sanha.

BEYONCE AJIFUNGUA MTOTO WA KIKE!!

Beyonce na Jay-Z wamepata mtoto wao wa kwanza, kulingana na ripoti kutoka Marekani
Taarifa hizo zilitolewa mara ya kwanza kwenye mitandao mbalimbali ya watu maarufu na kuthibitishwa kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter na marafiki wa wasanii hao maarufu, akiwemo Rihanna na Gwyneth Paltrow.
Taarifa zinasema mtoto huyo wa kike, Blue Ivy Carter, alizaliwa kwa njia ya upasuaji siku ya Jumamosi.
Hata hivyo, mpaka sasa wanandoa hao hawajathibitisha rasmi kwa kauli yao kuzaliwa kwa mtoto huyo.

Sunday, 8 January 2012

PILI HASSAN: ANATOKA MBAGALA ANATISHA KWA NGOMA ZA KIDOSI!!

INGAWA Pili sio maarufu katika ulimwengu wa sanaa, umahiri wake katika michezo ya mnyumbuliko wa mwili unampadisha chati katika sanaa za majukwaani zenye asili ya Kihindi. 

Hivi karibu Pili alikuwa kivutio kikubwa pale alipotokeza jukwaani katika kituo cha Utamaduni wa India akiwa miongoni mwa wasanii wa Kikundi cha Sanaa cha Jumuiya ya Wahindi Dar es Salaam (Banga Sangho) kuadhimisha miaka 150 ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mwanafalsafa Rabindranath Tagore. 

Pili ambaye alikuwa amevalia mavazi ya Kihindi alicheza kwa umahiri mkubwa wakati wa 
onesho lililoambatana na wimbo wa Rabindra Sangeet. Umahiri wake uliwafanya watazamaji 
waamini kuwa alikuwa mtu mweusi mwenye asili ya Asia. 

Hata hivyo baada ya onesho hilo kiongozi wa kikundi hicho alimtambulisha pili kuwa ni 
msanii wa Kitanzania na alialikwa kwenye onyesho hilo ili kuonesha jinsi mwanafalsafa Togore 
alivyotabiri juu ya maendeleo na changamoto zinazowakabili Waafrika. 

Pili alitumia fursa hiyo kuonesha kipaji chake katika kucheza ngoma na kuimba nyimbo zenye 
mahadhi ya Kihindi. Pili ambaye ni msanii katika kundi la Sanaa la Lumumba anasema yupo tayari kujifunza zaidi kuhusu sanaa za maonesho ya jukwaani na utamaduni wa watu wa Asia kwa lengo la kuwafundisha vijana wa Kitanzania wenye shauku ya kucheza ngoma za Kihindi. 

“Lengo langu ni kuwa mwalimu wa sanaa za majukwaani kwa kuwafundisha vijana wa 
Tanzania ngoma na nyimbo za Kihindi… hii itasaidia kuimarisha uhusiano wa Kiutamaduni kati ya India na Tanzania. Pia itakuwa sehemu ya kupanua soko la ajira katika fani ya sanaa,” anasema Pili. 

Anafafanua kuwa sanaa za maonesho ya jukwaani ni miongoni mwa fursa zinazowapatia 
wasanii kipato hivyo maonesho na muziki wenye hadhi ya Asia unaweza kuwavutia watu wengi 
zaidi. 

Ingawa kuna dhana kuwa watu wenye asili ya Asia hawapendi kuchanganyika na Watanzania wenye kipato cha chini, Pili anasema alifuatwa na kiongozi wa kikundi cha sanaa cha Jumuiya ya Wahindi wanaoishi Dar es Salaam na kumuomba ashiriki katika tamasha hilo la kumuenzi Tagore ambalo lilifanyika sanjari na maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika. 

“Sikupenda kupoteza nafasi hiyo hivyo nilikubali ombi hilo na kwenda nyumbani kwao. 
“Ingawa nilifanya mazoezi kwa muda mfupi tuliweza kucheza kwa ustadi mkubwa na mwalimu mwenye asili ya Asia anayeitwa Buri Buri ambaye alitufundisha kwa siku tatu kabla ya kujiunga na kundi la sanaa la ….kufanya mazoezi ya pamoja,” anaeleza. 

Nyota ya pili katika sanaa ya maonesho ya jukwaani ilianza kuonekana angali mtoto. Alijiunga 
na kundi la sanaa mara baada ya kujiunga na Shule ya Msingi Nzasa iliyoko Mbagala, Dar es 
Salaam ambapo alishiriki kuimba kwaya ya kucheza ngoma za asili katika kundi la shule. 

Baada ya kubaini kuwa shule yake haimpi fursa ya kutosha kuendeleza kipaji chake, aliomba 
kuhamia Shule ya Msingi ya Lumumba ambapo alipokelewa bila ya matatizo. 

“Awali nilikuwa naimba na kucheza ngoma za asili, lakini nilipohamia Lumumba nilipata fursa za kuongeza ujuzi kwa kujifunza kupiga marimba, gita (solo) na ala zingine za muziki. Pia nilijifunza kucheza dansi,” anasema. 

Anasema mafanikio aliyofikia katika sanaa yanatokana na juhudi zake pasipo kuungwa mkono na wanafamilia kwa kuwa wakati yeye alikuwa anaweka mikakati ya kuingia kwenye masuala 
ya urembo, familia yake ilitaka awe askari wa Magereza. 

“ Familia ilikutana niwe askari wa Magereza, mimi nilikuwa na malengo mengine tofauti hivyo 
nilipata wakati mgumu pale nilipoeleza kuwa lengo langu la kujikita katika kwenye masuala 
ya sanaa,” anaeleza. 

Hakuwa tayari kujiunga na Jeshi la Magereza kwa sababu alikuwa ameshaonja matunda 
yanayotokana na kazi ya sanaa ya maonesho ya jukwaani. Wakati akiwa wanafunzi wa shule ya 
msingi alikuwa akipata Sh 20,000 hadi 30,000 kwa mwezi kutokana na ushiriki wake katika kazi za sanaa. 

Kila alipopata fedha alimpelekea mama yake na kuamini zingeweza kumshawishi mama yake ili amuunge mkono katika mikakati yake ya kujiendeleza katika fani ya sanaa. 

Hata hivyo mambo yalikuwa tofauti, kwa kuwa mama yake hakuwa tayari kumuunga mkono hali ambayo ilisababisha kukabiliana na wakati mgumu kutokana na mvutano uliojitokeza mara baada ya kuhitimu elimu ya msingi. 

Anasema, “nilipata wakati mgumu hasa wakati wa kuaga kwa ajili ya kwenda kwenye mazoezi…. hakuna aliyeamini sanaa ni kitu chema na kinachoweza kumpatia mtu ajira…. nilichofanya ni kuhakikisha natekeleza mapema majukumu yangu ya nyumbani,” anasema. 

Kwa kuwa alilazimika kufanya kazi za nyumbani kwa wakati alilazimika kusonga ugali wa mchana saa nne asubuhi na kuuweka katika chombo kinachohifadhi joto na kisha kuondoka 
kwenda mazoezini. 

Pili aliendelea kujikita katika sanaa na hivi karibuni alifanikiwa kuwa miongoni mwa washiriki 14 walioingia kwenye fainali za shindano la dansi la Serebuka. Pili ni mahiri katika mchezo 
wa kunyumbulisha mwili hasa kuchezesha mabega, mikono na miguu, kucheza muziki wa dansi 
wa asili ya Afrika, India pamoja na ngoma za makabila mbalimbali nchini Tanzania. 

Anasema mwaka huu alikuwa miongoni mwa walimu waalikwa aliyepata nafasi ya kuwafundisha washiriki wa shindano la Tikisa katika mnyumbuliko wa mwili. 

Pili alijiunga na kundi la Lumumba baada ya kuhitimu elimu ya msingi mwaka 2005 anasema kuwa fani hiyo imempa mafanikio makubwa sana katika maisha yake, ikiwa ni pamoja na kufanya ziara katika nchi mbalimbali za Afrika na Ulaya kushiriki sanaa za maonesho ya jukwaani. 

“ Sanaa imeniwezesha kutembelea nchi za Denmark, Uganda, Kenya Msumbiji kushiriki katika 
shughuli mbalimbali za sanaa ambazo zote zimeniingizia kipato kilichonifanya nibadilishe maisha yangu,” Pili anafahamisha. 

Hata hivyo anasema hakuna kazi rahisi kwa kuwa anakumbana na changamoto mbalimbali 
ikiwa ni pamoja na dhana potofu ambayo husababisha kazi za sanaa kudharauliwa badala ya 
kuiangalia kama kazi ngingine. 

“Unaweza kupata kazi, lakini linapokuja suala la malipo, wanataka wakulipe kidogo bila 
kujali thamani ya kazi, hawajui hata wasanii tunatumia akili, muda na vifaa vinavyohitaji ukarabati kila kukicha,” Pili analalamika. 

Changamoto nyingine inayomkabili Pili inatokana na baadhi ya watu wenye dhana potofu 
kuwahusisha wanawake wasanii na ukahaba. 

“Wakati mwanamke anapofanya onesho zuri jukwaani anaweza kujitokeza mwanamume na kwenda kumtunza kisha kutumia nafasi hiyo kumtomasatomasa …wengine kuandika kwenye vikaratasi kuomba miadi ya kufanya mapenzi na pia wapo wanaoomba namba za simu ili kuweka miadi ya mapenzi,” anaeleza. 

Anasema jambo hili linamkwaza na siku zote huwa anajiuliza,” hivi hawa watu wananiona 
mimi malaya?” Anawasihi watu wenye dhana potofu juu ya wasanii wa kike waache vitendo vya udhalilishaji na hasa kutumia nafasi ya kumtunza msanii kama mwanya wa kuwashikashika wasanii wanapokuwa majukwaani. 

Hata hivyo anasisitiza kuwa changamoto hizo hazitamshawishi kubadilisha fani na badala 
yake atasonga mbele ili kufikia lengo la kuwa mwalimu wa sanaa na hasa kuwafundishwa watoto ngoma za asili kutoka ndani na nje ya nchi. 

Pili ambaye hivi leo anasherehekea kumbukumbu ya kuzaliwa kwake aliyezaliwa mwaka 1988 
akiwa mtoto wa nne kati ya saba. Ingawa hakubahatika kuendelea na elimu ya sekondari amebahatika kujiunga na kozi za Kiingereza, utamaduni na sanaa ya maonesho ya jukwaani ambapo ilimchukua miaka mitano kufuzu kozi ya sanaa ya kunyumbulisha mwili.

KAROLI STEPHEN, MKOMBOZI WA VIJANA KATIKA UFUNDI STADI!!

NILIPOACHISHWA kazi nilichanganyikiwa na kudhani ndio mwisho wa maisha…lakini tatizo
la ukosefu wa ajira kwa vijana ulinipa msukumo wa kuanzisha chuo cha ufundi stadi na kutumia elimu na ujuzi wangu kuendelea kulitumikia taifa kupitia sekta binafsi,” anasema Karoli Stephen.

Stephen ambaye hivi sasa ni Mkurugenzi wa chuo cha ufundi stadi kinachojulikana kama Metro Institute of Technology kilichopo Tanga, alianzisha chuo hicho baada ya kupoteza ajira yake serikalini mwaka 1999.

Awali Stephen alikuwa Mkufunzi katika Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), kituo cha Tanga na baada ya kuachishwa kazi, wanafunzi kutoka viwandani na vyuoni walikuwa wakimfuata na kumuomba awafundishe kwa kuwa hawakuwa na mwalimu.

“Nilipowaambia sina pa kufundishia waliamua kukodi darasa kisha kunisihi nikawafundishe kwa sharti la kuwatoza kiasi kidogo cha ada ili niweze kulipia pango na kujikimu,” anasema.

Baada ya kupata changamoto hiyo, mwaka 2000 alifanikiwa kupanga katika jengo la CCM lililopo eneo maarufu kwa jina la Kwa Kwaminchi na kuanzisha chuo alichokiita Amani Training Institute.

Hata hivyo, muda mfupi baadaye alijikuta akilazimika kulihama eneo hilo kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi waliokuwa wanamimimika kupata elimu ya ufundi stadi. Mwaka 2001 alihamia majengo ya NMC Gofu kisha kuunganisha nguvu ya taasisi mbili yaani Amani Training Institute na Nyerere Youth Centre, muungano uliozaa chuo cha Metro Institute of technology.

Umati wa wanafunzi walioendelea kumiminika kwenye chuo chake ulimpa wakati mgumu, kiasi
cha kuanza mchakato wa kutafuta eneo kubwa zaidi. Akiwa katika mchakato huo, mwaka 2007 alilazimika kufunga chuo hicho kwa muda.

Alikifungua tena mwaka 2010 baada ya kupata eneo kubwa katika moja ya majengo ya Bandari ya Tanga ambako ameyaboresha baada ya kuingia nao mkataba wa muda mrefu.
Anakiri kwamba, kwa sasa ana eneo kubwa, hivyo kuwafanya wanafunzi kujifunza fani zaidi ya
kumi bila ya kulazimika kubanana.

“Tumefanikiwa kuongeza idadi ya fani hadi kufikia kumi ambazo ni ufundi magari, umeme wa magari, uungaji wa vyuma, useremala, uashi, umeme wa majumbani, udereva, kompyuta, ushonaji wa nguo na upambaji,” alisema na kuongeza kuwa, chuo kimejikita katika fani mbalimbali ili kuwapa vijana fursa ya kujiendeleza na kuweza kujiajiri baada ya kuhitimu.

Anasema: “Tatizo la ukosefu ajira kwa vijana limekuwa kubwa na ni bomu linaloweza kulipuka
wakati wowote hivyo chuo kimeamua kushirikiana na wadau wengine kupunguza tatizo hilo kwa kutoa elimu ya ufundi stadi na kuhimiza vijana wajiajiri.”

Ili kuondokana na kero inayowapata wahitimu wanaokosa ajira kwa kisingizio cha kukosa uzoefu, chuo hicho kimeweka mpango unaowawezesha wanafunzi kwenda maeneo mbalimbali kufanyakazi ili kuimarisha mafunzo kwa vitendo na kupata uzoefu katika fani ya umeme wa majumbani, kompyuta na mapambo.

“Dhamira ya chuo hiki ni kuhakikisha vijana wananufaika na elimu ya ufundi ili kuwa chachu ya maendeleo katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia kwani bado tupo nyuma sana katika elimu ya ufundi” anasema,” Stephen ambaye chuo chake kinatoa mafunzo muda mfupi na muda mrefu.

Muda mrefu ni pamoja na ile ya mwaka mmoja inayojumuisha mafunzo ya udereva na ufundi ambazo humuwezesha mwanafunzi kufanya mitihani ya Trade Test na CBE inayotolewa na VETA.

Kozi ambazo zinachukua mwezi mmoja na nusu na zile za wiki mbili ni pamoja na udereva wa awali na mafunzo ya kompyuta kwa wale wanaojiendeleza bila kufanya mitihani ya VETA.

Chuo hicho kimefanikiwa kuongeza kiwango cha ufaulu katika programu za mitihani ya Trade
Test inayotolewa na VETA, ambapo ufaulu huo umeongezeka hadi kufikia asilimia 82.3 ya wanafunzi wote walioandikishwa.

Ufanisi huo unatokana na mkakati wa chuo wa kukuza kiwango cha ufaulu kwa kuajiri walimu
wenye elimu na uzoefu wa kutosha katika nyanja mbalimbali, miundombinu mizuri, na vitendea kazi vya kutosha ikiwa ni pamoja na magari ya mafunzo ya udereva na zana za ufundi.

Pia chuo hicho kinatumia kaulimbiu inayosema “Umahiri unaouzika” ikiwa na maana ya
kuongeza elimu na maarifa ili kuibua vipaji na mambo halisi ambayo hayafahamiki katika ufundi stadi.

Anasema ufaulu wa mitihani kwa wanafunzi wa chuo hicho unatokana na ushindani wa kuonesha kwa vitendo uwezo na umahiri wa kila mwanafunzi kudhihirisha kama alielewa ipasavyo mafunzo ya nadharia na kutumia elimu yake kutatua matatizo kwa kutumia fani au
ufundi stadi.

“Hatutaki mwanafunzi ahitimu katika chuo chetu akiwa na chochote alichojifunza, bali atoke akiwa ameiva na kumudu ushindani wa soko la ajira kwa kufanyakazi kwa umahiri wa kiwango cha juu,” anasema Stephen.

Mkurugenzi huyo aliyeonesha mfano wa kutokata tamaa baada ya kupata matatizo, ikiwa pamoja na kufukuzwa kazi, anasema chuo chake kwa sasa kinakabiliwa na changamoto ya kukamilisha azma ya kutekeleza kauli mbiu ya ujuzi unaouzika kwa kuwa maendeleo ya
sayansi na teknolojia yanakwenda kwa kasi ikilinganishwa na mabadiliko ya mitaala ya mafunzo ya ufundi pamoja na masharti ya kisheria ambayo yanalazimisha kufuata mitaala
inayotolewa na mamlaka ya elimu ya ufundi stadi.

Ameitaja changamoto nyingine kuwa ni gharama kubwa ya mafunzo ya ufundi stadi akisema elimu ya vitendo inahitaji vifaa vya kisasa ambavyo wanafunzi wa familia ya kipato cha chini haiwezi kumudu kuvinunua.

Kutokana na hali hiyo, anasema hali hiyo inachangia kukwamisha jitihada za chuo hicho kufikia malengo waliyonayo hivyo wanaiomba Serikali, wafadhili na wadau na katika maendeleo ya ufundi wajitokeze ili kukisaidia chuo hicho kiweze kuondokana na changamoto
hizo.

Stephen anasema pamoja na changamoto mbalimbali, chuo chake kinaweka mikakati ya kupanua huduma na katika miaka mitano ijayo kitakuwa na uwezo wa kusajili wanafunzi 600 kwa mwaka badala ya wanafunzi 100 wa sasa.

Pia chuo hicho kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kina mkakati wa kutoa mafunzo ya elimu ya sekondari hususani kwa watu wazima wanaotaka kufanya mitihani ya kidato cha nne na sita.

Anasema chuo chake kimefikia uamuzi huo baada ya kubaini kuwa kuna watu wengi wanaotaka kufanya mitihani ya sekondari ili kuboresha viwango vyao vya elimu. Anawahimiza watu wenye elimu na uwezo wa kuchangia taifa wasisubiri kuajiriwa serikalini badala yake wajiunge na sekta binafsi kwa kujiajiri wenyewe na kuajiri watu wengine kwa kuwa jambo hilo linawezekana.

Stephen amepata elimu ya awali katika shule ya msingi katika Shule ya Msingi Ndekeli mwaka
1979 na kujiunga Shule ya Ufundi Ifunda, mkoani Iringa ambako alihitimu mwaka 1983 na baadaye alisoma Chuo cha Ufundi Arusha alikohitimu mwaka 1986.

Miaka minne baadaye aliajiriwa na Ofisi ya Rais, Idara Kuu ya Utumishi na kupangiwa kufanya kazi Wizara ya Kazi hadi mwaka 1993 alipopata fursa ya kujiunga na Chuo cha Chang’ombe, Idara ya Taifa ya Mafunzo ya Ufundi Chang’ombe (NVTD) kuchukua mafunzo ya ualimu.

Ingawa Stephen amejikita katika ufundi anapenda kujishughulisha na kilimo,kusoma, kujifunza
maandiko matakatifu katika biblia na kufanya mazoezi.

WAHUJUMU UCHUMI WAKIONA CHA MOTO!!

VIONGOZI wanne wa Serikali ya kijiji cha Mkwakwani kilichopo Kata ya Mnyuzi wilayani Korogwe wameswekwa rumande kwa kuwadanganya wananchi kwamba wametumwa na Mkuu wa mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa wakate miti saba aina ya mivule kutoka kwenye Pori la Akiba la Manta ili kupata mbao za kupaulia jengo la Zahanati na vyumba vya madarasa. 

Viongozi hao ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mkunguni, Festo Nyika, Katibu wa Kamati ya 
Ulinzi na Usalama katika kijiji cha Mkwakwani, Joseph Kimako, Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho, Manyirizi Method na Mlinzi wa Msitu (pori) wa Manta, Ayubu Nyika. 

Kukamatwa kwa viongozi hao waandamizi katika serikali ya kijiji hicho kunafuatia agizo lililotolewa na Mkuu wa Mkoa mara baada ya kufanya ziara ya kushitukiza kijiji hapo. 

Taarifa zinasema viongozi wa serikali ya kijiji hicho walidai kwamba wametumwa wakate 
miti hiyo ambayo baada ya kuipasua walipata mbao zaidi ya 300 ambazo walizisafisha na 
kutelekeza 40 kijijini hapo. 

“Ziara yangu ya leo hapa kijijini ni mahsusi kwa ajili ya viongozi wenu waliowadanganya kuwa 
nimewatuma mimi pamoja na mkuu wa Wilaya, Erasto Sima waje kuvuna miti ya mbao hapo 
msituni, taarifa hizo si za kweli na hao watu ni waongo, siwafahamu na sijawahi kuwatuma kwenu. 

“Kutokana na udanganyifu na uhalifu uliofanywa na viongozi wenu hao nataka kamati ya ulinzi 
na usalama ya wilaya ihakikishe inawasaka hadi kuwakamata na kuwaweka chini ya ulinzi tena 
ndani ya saa 48 kuanzia sasa hivi (jana) ili hatua nyingine za kinidhamu na kisheria ziweze 
kuchukuliwa dhidi yao”, aliagiza Gallawa. Walikamatwa baadaye na kuswekwa rumande.

HIVI KWANINI HUYU AKICHAPWA HAKOSI LA KUSEMA?

Chama cha ndondi duniani ' World Boxing Association' kimeamuru pambano kati ya Amir Khan na Lamont Peterson lirudiwe bila kupoteza wakati, kwa mujibu wa ma promota wa Khan.
Peterson na Khan
Peterson na Khan
Khan alipoteza mataji yake mawili la WBA na IBF kwa Lamont Peterson mwezi disemba lakini akahoji masuala kadhaa yaliyotokea wakati pambano hili likiendelea.
Moja ya madai ni kwamba kuna mtu mmoja ambaye hakutambulika, na sasa amefahamika ni nani, aliyeonekana kuingilia shughuli za mwamuzi mmoja wa WBA.
"kutokana na hilo sasa WBA...itaamuru pambano hilo lirudiwe, amesema Mkurugenzi wa kampuni ya Golden Boy Promotions, Richard Schaefer.
Mkuu huyo amesema kua "tumepokea risala ikithibitisha habari hizo mapema leo jumamosi na ujumbe wa mandishi utatufikia jumanne ijayo.
"hiyo ina maana kua wapiganaji hawa wawili hawawezi kushiriki pambano lolote kabla ya pambano la marudiano. Hivyo ndoto za Peterson ya kutaka apambane na mtu mwingine kujizidishia kipato na sifa zimefifia.
Mkurugenzi wa Golden Boys anasema wanataraji Chama cha IBF nacho kitakubaliana na uwamuzi wa WBA.
Hapo awali, Rais wa WBA Gilberto Mendoza ameiambia BBC michezo kua, hali hii inazua mizengwe na hivyo inabidi pambano lirudiwe kuondoa mashaka.
Halimashauri ya ndondi ya Washington imelaumiwa kwa kutofuata utaratibu unaostahiki pambano kama hilo.
Khan alipoteza pambano hilo la uzani wa light-welterweight kwa pointi chache baada ya kupokonywa pointi zake mbili kwa kumsukuma mpinzani wake.
Amir Khan na taji moja
Majaji George Hill na Valerie Dorsett waliamua pambano hilo 113 kwa 112 kwa Peterson, huku Jaji mwingine Nelson Vasquez akimpa Khan ushindi wa 115-110.
Kwa mujibu wa maandishi ya kadi ya Hill imeonekana kua uwamuzi wake wa awali Khan alishinda raundi ya saba lakini baadaye alibadili uwamuzi na kumpunguzia Khan pointi na hivyo Peterson kupata ushindi wa 10-8, jambo ambalo bila mabadiliko ya baadaye ya Jaji Hill Khan angeibuka mshindi wa pambano hilo.

VIBULUDISHO KWA WADAU WOOTE!!

Mwizi na 'haja'

DNA
Teknolojia ya DNA
Mwizi mmoja nchini Uchina aliyekuwa na tabia ya kujisaidia haja kubwa katika nyumba anazofanywa wizi wake, hatimaye amekamatwa kutokana na teknolojia ya DNA.
Polisi jijini Cixi, katika jimbo la Zhejiang wamesema mwizi huyo aitwaye Chen mwenye umri wa miaka 29 akiwa na mwenzake walivunja nyumba moja na kuingia jikoni na kula chakula, kabla ya bwana Chen kujisaidia kwenye sakafu karibu na mlango.
Baada ya kufanya hayo, wawili hao wakaanza kutafuta vitu vya kuiba ndani ya nyumba hiyo, lakini kutokana na kukuru kakara zao, mwenye nyumba alishtuka, na wezi hao kukimbia bila ya kuiba chochote. Miezi michache baadaye, wezi hao waliingia katika nyumba nyingine na kuiba kompyuta mpakato-- yaani Laptop na fedha taslimu yuan elfu moja.
Kama kawaida, waliingia jikoni na kujipakulia chakula, na bwana chen kuacha muhuri wake wa kawaida, wa kinyesi chenye harufu kali karibu na mlango wa mbele. Mtandao wa china daily umesema polisi walifanikiwa kulinganisha vipimo vya DNA na mwizi Chen, ambaye aliwahi kutupwa gerezani kwa kosa jingine mwaka 2003. Baada ya kukamatwa, bwana Chen alikiri kujisaidia katika nyumba anazofanya wizi, akisema, amekuwa akisoma katika vitabu mbalimbali jinsi wezi wanayokuwa na mitindo yao ya kipekee, wanapofanya wizi. Polisi bado wanamsaka mwizi mwenzake.

Mwizi arejesha alichoiba

Zawadi
Zawadi za Krismasi

Bwana mmoja aliyeiba zawadi za Krismasi katika nyumba moja nchini Marekani, amerejesha zawadi zote, na kuandika ujumbe wa kuomba radhi. Mike Valloney aliyeibiwa zawadi hizo amesema camera zake zilimrekodi mwizi huyo akiiba. "Alikuwa akitazama huku na huko, akihisi kama kuna mtu anamtazama" amesema bwana Mike.
Hata hivyo kituo cha televisheni cha WPIX kimesema siku mbili baada ya kuiba zawadi hizo, mwizi huyo alirejea tena, na kurudisha kila alichoiba.
Aidha, mwizi huyo pia aliandika ujumbe usemao " Naomba radhi. Heri ya mwaka mpya. Nataka kufanya mambo mazuri mwaka huu" umesema ujumbe huo. Bwana Valloney aliyeibiwa amesema hadhani kama mwizi huyo ataiba tena.

Aiba na kumuuzia aliyemuibia

iPhone
iPhone kama hii

Polisi mjini Florida Marekani wamesema wamemkamata mwizi mmoja aliyejaribu kumuuzia vitu mtu aliyemuibia vitu hivyo.
Polisi katika kiunga cha Miramar, Florida wamesema mwizi huyo baada ya kuiba simu aina ya iPhone na tabiti aina ya iPad, alimpigia alyemuibia siku mbili baadaye akitaka kumuuzia vifaa hivyo hivyo alivyomuibia.
Polisi wa Miramar wamesema bwana Hank Yan aliyeibiwa siku ya Jumatatu, alishikiwa bunduki na watu wawili waliompora simu na tabiti pamoja na dola mia tano taslimu, limeripoti gazeti la South Florida Sentinel. Polisi wamesema bwana Yan alipokea simu siku mbili baada ya kuibuiwa na alitambua sauti ya mtu anayetaka kumuuzia iPad, na hivyo kupanga kukutana naye. Wezi hao, Zachari Swindle na Devonte Suckie walikamatwa na polsi walipojitokeza katika mahala walipokubaliana na mteja wao.

Bibi na bangi

Bangi
Miche kadhaa
Mwanamama mmoja mwenye umri wa miaka sitini na saba nchini Marekani, ameachiliwa huru na mahakama baada ya kushtakiwa kwa kosa la kupanda miche ya bangi katika bustani yake.
Makachero wa polisi wamesema walikuta miche saba yenye afya na yenye urefu wa futi nne katika bustani ya mwanamama huyo mjini Uniontown, Philadelphia. Mama huyo aitwaye Alberta Kelly amesema yeye alirusha mbegu tu kwenye bustani yake baada ya kupewa mbegu hizo na mtu mmoja mwenye madevu lakini asiyemfahamu.
Bi Kelly amesema wala hakufahamu kama ni bangi, na mtu aliyempa mbegu hizo alimwambia ni mbegu za maua. Bi Kelly alikiambia kituo cha Televisheni cha WTAE kuwa majani ni majani tu.

Hujui Beyonce kaolewa na Jay Z?

Beyonce
Beyonce kaolewa na Jay Z
Polisi mjini Parma, Ohio, nchini Marekani wamesema mtu mmoja amechomwa kisu kwa sababu tu hakuwa akifahamu kwamba mwamamuziki Beyonce ameolewa na msanii Jay Z.
Kachero wa polisi Marty Compton wa kituo cha polisi cha Parma amesema mtu mmoja aitwaye Garfield Heights siku ya mwaka mpya alikuwa akibishana na Ronald Deaver, baada ya bwana Deaver kugundua kuwa Bwana Garfield hafahamu kuwa wanamuziki hao mashuhuri wa Marekani ni wanandoa, kimeripoti kituo cha TV cha WJW, siku ya Alhamisi.
Kachero Compton amesema Bwana Deaver alimchoma kisu bwana Garfield nje tu ya nyumba yake majira ya saa tano usiku saa za huko. Bwana huyo aliyechomwa kisu imeripotiwa anaendelea vizuri katika hospitali ya Metro mjini humo alipolazwa.
Bwana Deaver alikamatwa na kushtakiwa kwa kosa la kushambulia.
-----------------------
Na kwa Taarifa yako...
Watu huzungumza takriban maneno mia moja na ishirini kwa dakika moja.

AMRI YA KUTOTEMBEA YAWEKWA NIGERIA!!

Mashambulio dhidi ya makanisa, Nigeria

Amri ya kutotoka nje wakati wowote ule imetangazwa katika jimbo la Adamawa, Nigeria, baada ya mashambulio kadha dhidi ya Wakristo.
Jeshi limeshika zamu mabarabarani, na taarifa kutoka mji mkuu wa jimbo, Yola, zinaeleza kuwa maduka na maofisi yote yamefungwa, na huduma za lazima tu ndio zinaruhusiwa.
Wafuasi wa kikundi cha Waisalmu wenye siasa kali, Boko Haram, wameshambulia kanisa, kituo cha jamii, na duka la msusi katika siku za karibuni, na kuuwa watu kama 29.
Sheria za dharura zilianzishwa katika majimbo kadha mengine ya kaskazini mwa Nigeria juma lilopita, ambako Boko Haram wamefanya mashambulio piya.
Kikundi hicho kimeuwa watu zaidi ya 500 katika muda wa mwaka.