PATA HABARI MOTO MOTO, ZA KITAIFA NA KIMATAIFA KUPITIA HAPA, TUPE MAWAZO YAKO TUYAFANYIE KAZI, TUPE HABARI ZOZOTE ULIZO NAZO TUTAZIWEKA HAPA,KWA MWENYE PARTY AINA YOYOTE INAYOHUSIANA NA MAMBO YA MUSIC, TAFADHARI ONGEA NA PAPAYA KUPITIA NAMBA HII..07501 202029..YUPO MACHO 24/7 BEI MAELEWANO.

Tuesday, 15 November 2011

MFUNGWA ALIYEACHIWA KWA MSAMAHA WA PAROLE AWA KINARA WA MAENDELEO


Mfungwa aliyepewa msamaha wa parole baada ya kutumikia theluthi ya kifungo chake cha miaka 15 kuua bila ya kukusudia, amekuwa kinara wa gurudumu la maendeleo katika Kijiji cha Mbirikili Wilaya ya Serengeti mkoani Mara.
Hayo yalibainishwa na wakazi wa kijiji hicho wakati mfungwa huyo, Chacha Kerenge, alipotembelewa na wajumbe wa Bodi ya Taifa ya Rarole nyumbani kwake ambako alifanyiwa tafrija ya kukubalika kijijini hapo na kuonyesha msukumo wa maendeleo kwa jamii tangu atoke gerezani .
Akizungumza kwa niaba ya wanakijiji wenzake, Mwita Ngoka, alisema kuwa Kerenge alipofika kijijini hapo, amekuwa mfano mzuri kwa jamii hususani vijana kwa kile alichodai kuwa hufanya kazi kwa juhudi katika kujitafutia riziki na maendeleo ya familiya yake.
Ngoka alisema kwa sasa katika kijiji hicho hakuna kijana anayetafuta maendeleo kwa bidii na kasi ya ajabu kama mfungwa huyo.
Alisema mfungwa huyo anamiliki mbuzi 54 na ng’ombe 16 na shamba la mazao lenye ukubwa wa hekari tatu.
Kwa upande wake mgeni rasmi katika sherehe hizo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Taifa, Ben Kaijage, aliiasa jamii kuwapokea wafungwa pale wanapopewa misamaha au wanapomaliza kutumikia vifungo gerezani kwa moyo mmoja na kuwapa ushirikiano.
“Mfungwa anapofungwa gerezani si kwamba hatakiwi kurudi tena kwa jamii la hasha, gerezani ni sehemu ya mfungwa kujutia makosa yake na kupata elimu ya kuishi vema katika jamii,na ndo maana wafungwa hupewa mafunzo mbalimbali wakiwa gerezani, ”alisema Kaijage.
Kaijage alisema mfungwa huyo alifungwa Septemba 25, mwaka 2003 katika Gereza la Butimba Mwanza na kuhamishiwa Gereza la Kilimo Mgumu Septemba 20, mwaka huo ambako alitumikia kifungo kwa miaka sita na kupata bahati ya kuchaguliwa kuingia katika msamaha huo wa parole.
Alisema mfungwa huyo alipewa msamaha wa parole mwaka 2009 na kuiasa jamii kuwakubali wafungwa kwa kile alichodai kuwa kuna baadhi wanapata bahati ya kuingia katika msamaha hiyo ili waende wakamalizie kifungo uraiani wakiwa na familiya zao.
Naye mfungwa huyo, alisema anaishukuru jamii kwa kumpokea kwa mikono miwili na kumpa moyo wa matumaini ya maendeleo yake.
Kerenge alisema anaiomba bodi hiyo ilegeze masharti ya msamaha wa parole kwa kile alichodai kuwa wapo wafungwa wengi waliopo gerezani wamekwisha kujutia makosa yao lakini hawana haki ya kujaza fomu ya kuomba parole kwa kuwa makosa waliyotenda hayaruhusiwi kupewa msamaha.
Alisema wapo wafungwa wengine wamefungwa kwa makosa ya kusingiziwa na makosa hayo ni moja wapo ya makosa ambayo hayana msamaha, hivyo kumnyima haki ya kupewa msamaha wa parole ni kumnyima haki ya msingi mfungwa.
“Mfano mzuri ni mimi,nilifungwa miaka 15 kwa kosa la kuuwa bila kukusudia lakini nilikuwa sijauwa ila nilifungwa bila kosa,kwa vile mauwaji hayo yalipokuwa yakifanyika nilikuwa katika eneo la tukio,na cha kushangaza nilikuwa nashtakiwa mimi peke yangu kuwa ndiye niliyeuwa,ila namshukuru mungu kwa kupata msamaha,” alisema Kerenge

SWAZILANDA YAHITAJI MABADILIKO

Mfalme Mswati III
Kiongozi mwandamizi wa Kianglikana wa Swaziland, Askofu Meshack Mabuza, ametoa wito kwa mfalme Mswati III kuachia madaraka ya kisiasa ili kuipa nafasi serikali ya kidemokrasia.
Askofu Mabuza ameiambia BBC mfumo wa serikali wa "mambo ya kale" umeiingiza nchi katika mgogoro mzito wa fedha na uchumi.
Taarifa ya serikali imesema mishahara kwa wafanyakazi wa serikali yatacheleweshwa mwezi huu kutokana na upungufu wa fedha.
Mfalme Mswati, mwenye wake 13, ni kiongozi pekee mwenye kushilikia mamlaka yote kusini mwa jangwa la Sahara.
Anashutumiwa kwa kiasi kikubwa kuhusishwa na ufisadi, lakini akaahirisha sherehe zake za kufikisha miaka 25 madarakani mwaka huu kutokana na msukosuko wa fedha nchini humo.
Mpaka sasa Swaziland imekataa kupokea mkopo wa dola za kimarekani milioni 355 kutoka Afrika kusini kuisaidia kulipa gharama mbalimbali, baada ya Pretoria kuitaka nchi hiyo kufanya mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi.

'Visababu'

Askofu Mabuza, askofu wa Kianglikana wa Swaziland, aliiambia BBC kuwa matatizo ya Swaziland hayatokwisha iwapo uongozi huo utaendelea kuwepo madarakani.
Alisema, "Jawabu kwa hakika litatokana na mabadiliko ya uongozi wa serikali ya kiutamaduni, kikabaila, na mambo ya kale."
"Lazima ibadilishwe na uongozi wa kidemokrasia wa vyama vingi."
Taarifa ya serikali iliyoonekana kabla ya kutolewa rasmi- iliyotiwa saini na mhasibu anayekaimu, AF Mabila- ilisema malipo ya mishahara ya wafanyakazi wa serikali ya Novemba imesogezwa hadi Desemba.
Msemaji wa serikali Percy Simelane aliiambia BBC baraza la mawaziri limekuwa likijadili suala hilo tangu Jumamosi, lakini mpaka sasa hamna muafaka wowote uliofikiwa.
Serikali imesema mgogoro wake wa fedha umesababishwa na msukosuko wa uchumi duniani na kuporomoka kwa mapato ya uongozi huo kutoka umoja wa ushuru wa forodha wa kusini mwa Afrika (sacu), kufuatia makubaliano mapya ya ushuru wa forodha mwingi.
Lakini askofu Mabuza, anayetarajiwa kuachia madaraka mwezi ujao, alisema hivyo ni "visababu".
Alisema, " Matatizo ya kiuchumi yalikuwepo hata kabla ya kuporomoka kwa uchumi wa dunia kwasababu imekuwa kama hakuna ukuaji wa kiuchumi."
"Nchi hii imefika hatua ya kuporomoka kabisa."
Kumekuwa pia na wasiwasi kuwa hospitali za taifa zinaweza kuishiwa na dawa za kufubaza ukimwi ARVs kutokana na upungufu wa fedha.
Swaziland, yenye jumla ya watu milioni 1.2, ni miongoni mwa nchi zenye idadi kubwa ya walioathirika na ukimwi duniani.
Takriban watu 230,000 wanaishi na virusi vya ukimwi, ambapo 65,000 wanategemea hospitali za taifa kuwapa dawa hizo za ARV.
Vyama vya kisiasa vinazuiwa Swaziland, ambapo Mfalme Mswati amekuwa madarakani tangu mwaka 1986.
Wakosoaji wanaishutumu familia hiyo ya kifalme kwa kuwa na matumizi makubwa kupita kiasi, licha ya idadi kubwa ya watu wake wakiishi maisha ya kimaskini.
Msukosuko wa kiuchumi umechochea maandamano dhidi ya uongozi wa mfalme Mswati, lakini wachambuzi wamesema ufalme huo bado unapewa heshima kubwa na Waswaziliand wengi wanaothamini mila na desturi zao.
Bobsam Elejiko afariki dunia uwanjani
Bobsam Elejiko afariki dunia uwanjani
Mchezaji wa nafasi ya ulinzi wa Nigeria Bobsam Elejiko, alianguka uwanjani na kufariki dunia wakati akiichezea timu yake ya Ubelgiji ya Merksem SC siku ya Jumapili.
Beki huyo mwenye umri wa miaka 30 alikuwa akicheza mechi dhidi ya FC Kaart wakati alipoanguka na kupoteza fahamu.
Majaribio ya kuuzindua moyo wake yalishindikana na sababu za kifo chake hazijaelezwa mara moja.
Taarifa iliyotolewa na klabu ya Merksem imesema:"Kwa masikitiko makubwa tunatangaza kifo kilichotokea ghafla cha Bobsam Elejiko." Mechi hiyo ilisimamishwa baada ya kifo cha Elejiko.
"Alianguka na kufa hapo hapo uwanjani na rambirambi zetu tunazitoa kwa familia yake na marafiki."
Elejiko alishawahi kuchezea klabu za Westerlo na Antwerp.

Sunday, 13 November 2011

ASPIRINI HUEPUSHA SARATANI


Wataalamu wa tiba wameshauri kua watu ambao afya yao inakabiliwa na uwezekano wa kukumbwa na saratani ya kibofu, wapewe dozi ya aspirini.
Jarida linalochapisha habari za utafiti wa wataalamu ''The Lancet'' limearifu kua tembe mbili kwa kila siku zilipunguza saratani ya kibofu kwa asili mia 63% kati ya kundi la wagonjwa 861.
Profesa Sir John Burn wa Chuo kikuu cha Newcastle, aliyeongoza utafiti huo anasema kua ushahidi walioupata umetoa changamoto kubwa kuhusu uwezekano huo.
Wataalamu wengine wamesema kua utafiti huo umetoa mwangaza mpya kwamba aspirini inaweza kutumika katika kutibu saratani kwa ujumla.
Utafiti huu ulifanywa kwa kutumia wagonjwa 861 waliorithi maradhi haya ya saratani ya kibofu, ambayo huathiri mtu mmoja kati ya watu 1,000.
Kuna tatizo la kugundua wagonjwa kama hawa waliorithi magonjwa kama haya na tiba ya viini vya urathi huwa kazi kubwa, ikimaanisha kwamba kuna uwezekano kwao kukumbwa na maradhi kama saratani ya kibofu, kizazi na tumbo.
Uchunguzi wa wagonjwa wote wakati wa majaribio, wale waliokua katika kundi lililopewa miligramu 600 ya vidonge vya aspirini kwa kila siku, 19 kati yao walipatikana na uvimbe ikilinganishwa na uvimbe uliopatikana miongoni mwa wagonjwa ambao walikua wakitazamwa kwa karibu sana, ambao kiwango cha uvimbe kilipungua kwa asili mia 44.

Wataalamu hawa walipochunguza wagonjwa pekee waliotumia dawa hii kwa kipindi cha miaka miwili wakakuta kuna upungufu wa asili mia 63%.
Vilevile tiba hii ina athari juu ya saratani nyingine za uruthi, ambazo pia zilishuka kwa kadiri ya nusu kwa wagonjwa wanaochunguzwa kwa makini.
Profesa Sir John Burn, kutoka Chuo kikuu cha Newcastle alisema kua watu wazima 30,000 nchini Uingereza walirithi saratani ya kibofu.
Profesa Burn aliongezea kusema kua ikiwa watu hao watapewa matibabu basi tutapunguza saratani elfu kumi katika kipindi cha miaka 30 na kuonelea kua hilo linaweza kuepusha vifo takriban 1,000 kutokana na maradhi haya.
Hata hivyo, kuna athari zake pia.
"tukiweza kupunguza saratani 10,000 na kuzusha madonda ya tumbo 1,000 pamoja na kuondoa mishtuko ya moyo 100, kwa fikra za watu wengi ni bora kuliko kusubiri vifo, alisema Profesa Burns.
"watu wenye asili ya familia ambayo huathiriwa na magonjwa ya aina hii, hususan saratani ya kibofu ingefaa wajaribu dozi ndogo ya asipirini kama tabia."
Tangu hapo Aspirini ina sifa ya kupunguza maradhi ya mshituko wa moyo na kiharusi.
Utafiti mwingine katika kipindi cha miongo miwili iliyopita umeonyesha kua dawa aspirini hupunguza hatari ya saratani, ingawa utafiti huu wa sasa ndio wa kwanza kwa kutumia wagonjwa katika majaribio na kuhakiki aspirini katika kutibu saratani.
Moja ya maswali yaliyoulizwa kuhusu utafiti huu ni kama watu ambao hawana matatizo ya afya wala familia zenye historia ya ugonjwa huo wanaweza kutumia dawa hii.
Jibu likawa kua matumizi ya aspirini yanapunguza uwezekano wa saratani na maradhi ya moyo, kwa hiyo ni vizuri lakini kuna athari zake pia. Kwa Profesa Sir John, ni hoja nzuri hio kwa sababu yeye binafsi anaonelea kua athari za dawa hio ikilinganishwa na kiwango cha kuepuka saratani na maradhi ya moyo ni ndogo.
Hata hivyo anaonya kua atakayeamua kutumia aspirini kuepusha balaa la saratani, kiharusi au maradhi mengine ya moyo lazima achukue tahadhari. Matumizi ya dawa hio huongeza uwezekano wa madonda tumboni, kutokwa damu ndani ya tumbo ingawa wataepuka kiharusi kwa kutumia aspirini."

SAMAHANI KWA WADAU WOTE, KWAKUA KIMIYA KIDOGO, BUT KWANZA IS BACK KWA HASIRA.


Kula ukiwa umevaa nguo

Moja ya jiji linalotajwa kuwa huru na lenye uvumulivu nchini Marekani, San Fransisco, sasa limeamua kuweka bayana kuhusu suala la watu kula chakula hadharani wakiwa hawajavaa nguo.
Bodi ya wasimamizi ya jiji hilo imeweka sheria mpya kukataza watu wasiovaa nguo kula katika migahawa, bila kufunika na vitambaa viti wanayokalia, limeripoti gazeti la San Fransisco Examiner.
Yeyote atakayekiuka sheria hiyo mpya atapigwa faini ya dola mia moja kwa mara ya kwanza, na dola mia mbili iwapo watarudia tena, na mara ya tatu atapigwa faini ya dola elfu moja au kwenda jela kwa mwaka mmoja. Watu kutembea bila nguo mitaani ni jambo linalovumilika mjini humo hasa katika eneo la Castro.

FLAT SCREEN GEREZANI


Polisi mjini Acapulco kusini magharibi mwa Mexico wamekuta wafungwa katika gereza moja wakiwa na televisheni mia moja, deki za DVD, magunia mawili ya bangi na majogoo mia moja.
Polisi wamesema televisheni hizo zilikuwa flat screen. Aidha wamesema wamekuta pia wanawake 25 wakiishi katika sehemu ya wafungwa wanaume, sita kati yao walikuwa wafungwa, lakini 19 waliosalia ni wahamiaji haramu, ambao vyombo vya habari vimeripoti kuwa ni makahaba.
"Hatimaye tumekamata wanawake 25 wakiwa wamevaa mawigi" Amesema Arturo Martinez, msemaji wa jimbo la Guerro. Majogoo mia moja waliokutwa ndani ya gereza hilo imeelezwa ni kwa ajili ya mchezo wa kuwapiganisha ambao ni maarufu katika eneo la Amerika ya Kusini.
Mkuu wa gereza hilo, mkuu wa usalama wa gereza na baadhi ya walinzi wa gereza hilo wamefukuzwa kazi.

111111

Kimamama waja wazito wanaokaribia kujifungua nchini Korea Kusini, walipeleka maombi ya kutaka kujifungua kwa kufanyiwa upasuaji siku ya Ijumaa, ili watoto wao wazaliwe, tarehe kumi na moja ya mwezi wa kumi na moja mwaka elfu mbili na kumi na moja.
Namba za utambulisho wa utaifa wa Korea Kusini zina tarakimu kumi na tatu, na tarakimu sita za mwanzo huwa tarehe ya kuzaliwa, na hivyo vitambulisho vya watoto hao vitakuwa na vikianza na namba 111111 na kufuatiwa na namba nyinginezo. Idadi ya kinamama waliotaka kujifungua mwaka huu ni asilimia 20 zaidi ya miaka mingine.
Kinamama ambao tarehe zao za kujifungua ni wiki moja baada ya tarehe kumi na moja wamesema wako tayari kujifungua mapema, limeripoti gazeti la Seoul. Wakati huohuo, mapacha wawili nchini Marekani walipanga kufanya sherehe kubwa ya kuadhimia miaka kumi na moja ya kuzaliwa, siku ya tarehe kumi na moja mwezi wa kumi na moja mwaka 2011.
Novemba kumi na moja ni maarufu nchini Korea Kusini ikijulikana kama siku ya Pepero, au siku tamu, sawasawa na siku ya wapendanao ya Valentine.

NYUKI

Zaidi ya nyuki elfu sitini wamekutwa katikia myumba ya bwana mmoja aliyekutwa amekufa nchini Marekani.
Mtandao wa news.com umesea bwana huyo amekufa kutokana na sababu zosizojulikana, lakini nyuki walikutwa wakiinshi ndani ya ukuta wa nyumba yake.
Mtu huyo ambaye hakuwa ametambuliwa alikutwa na mwanaye wa kike, kimeripoti kituo cha TV cha WPLG. Mtaalam wa nyuki Willie Sklaroff ambaye ataondoa nyuki hao amesema wako karibu elfu sitini.
Taarifa zinasema bwana huyo alikuwa akikarabati nyumba hiyo kwa ajili ya kumpa mwanaye wa kike, lakini pia haifahamiki kama alikuwa akiwafuga nyuki hao, au hata kama alikuwa akifahamu kama wanaishi nyumba moja.

KADI NYEKUNDU KWA KUVAA NYEKUNDU

Mwamuzi mmoja wa soka hapa Uingereza alitoa kadi nyekundu kwa wachezaji sita kwa sababu ya rangi ya nguo zao za ndani.
Tukio hilo liliokea Wales ambapo mwamuzi aligundua mchezaji wa timu moja alikuwa amevaa nguo nyeupe ya ndani huku bukta yake ikiwa rangi nyekundu, limeripoti gazeti la Bath Cronicle.
Mchezaji mwingine alionekana na mwamuzi huyo akiwa kavaa nguo ya ndani ya rangi nyeusi. Mchezo huo ulikuwa kati ya timu moja ya England ikipambana na Bath City ya Wales.
Sheria za chama cha soka cha England zinasema wachezaji wanatakiwa wavae rangi zinazifanana za nguo za ndani na nje. Hata hivyo sheria hiyo huwa haizingatiwi sana.
Kuongeza utata, refa huyo aliwataka wachezaji wawili kubadili nguo zao mbele ya mashabiki, na wakati wawili hao wako nje, timu yao ikafungwa bao moja.
Timu hiyo iliishia kuchapwa mabao 6 kwa bila.

Na kwa taarifa yako...

Chuma huwa kizito zaidi kikipata kutu

Wednesday, 2 November 2011

MISHA B, BADO ANAKOMAA NAO

Misha B, X Factor 2011Misha B has refused to publicly forgive X Factor judge Tulisa Contostavlos (Picture: KMK)

Misha, who survived a tearful sing-off against Sophie Habibis on Sunday, had to be calmed down by friends backstage.
She also refused to publicly forgive judge Tulisa Contostavlos, who painted a ‘mean’ picture of her the week before. 
The bewildered 19-year-old snapped ‘no comment’ when she was asked to respond to Contostavlos’s claims the pair had ‘sorted out’ their feud.
While the hopeful was showing restraint, Gary Barlow pointed the finger firmly in the direction of the N-Dubz star Contostavlos for dredging up backstage gossip about Misha.
‘All the antics last weekend must have had an effect on her (Misha) because the song was amazing, her voice is incredible, her version of that track this week absolutely off the scale,’ said the 40-year-old Take That legend.
It later emerged that croaky Kelly Rowland had forgiven Contostavlos in a peace call from her sick bed in America moments before she joined in the vote off by phone. 
But she would have been unaware at the time how far her frontrunner Misha B’s popularity had been blighted.
Misha dried her tears vowing the only way back was to convince viewers she is the same person backstage as in front of the cameras.
‘It’s down to the public vote,’ she told me. 
‘I take responsibility for my own actions. I am just going to continue to keep doing what I love, which is performing and celebrating good music,’ she said.


Read more: http://www.metro.co.uk/tv/880313-misha-b-breaks-down-backstage-as-x-factor-dream-turns-sour#ixzz1cVxt7zld

THE X FACTOR USA, HUYU DOGO NI NOOMA, WASHA MPA JINA LA JAY Z.

Wadadaz kama kawaida yao washaanza kumlia mingo. aka. kumtega

CHEKA UKIONA PANA CHEKESHA, KAMA HAPACHEKESHI HUZUNIKA


Msichana ageuka punda?

Bwana mmoja nchini Zimbabwe amedai kuwa kahaba aliyekuwa akifanya naye mapenzi amegeuka ghafla na kuwa punda.
Bwana huyo, Sunday Moyo ambaye amefikishwa mahakamani siku ya Jumatatu kwa kosa na kukutwa akifanya mapenzi na mnyama huyo amesema anampenda sana mpenzi wake huyo. Bwana Moyo aliiambia mahakama mjini Zvishavane kuwa huyo waliyemkuta naye sio punda bali ni mwanamke ambaye alikutana naye katika klabu ya usiku ya starehe.
Gazeti la Metro limesema polisi wa Zimbabwe wakiwa katika doria saa za alfajiri, walimkuta bwana huyo mwenye umri wa miaka 28, katika mji wa Mandava, akifanya mapenzi na punda nje ya nyumba yake. Mnyama huyo alikuwa amelala chini huku shingo yake ikiwa imefungwa kamba, na kamba hiyo kufungwa kwenye mti. Kwa mujibu wa mtandao wa New Zimbabwe.com bwana Moyo amekiri makosa ya kujamiiana na mnyama, lakini aliiambia mahakama kuwa "Mheshimiwa Jaji, niligundua tu kuwa ni mnyama, wakati polisi waliponikamata". Bwana huyo amesema alipata kahaba aliyekubali kulipwa dola ishirini, lakini amesema hafahamu ilikuwaje hadi akageuka na kuwa punda. "Lakini bado nampenda sana" amesema bwana Moyo. Bwana huyo ameswekwa rumande na kuamriwa kufanyiwa uchunguzi wa akili.

Mke arudi ghafla

Bwana mmoja aliyealika msichana nyumbani kwake, wakati mkewe hayupo, alimkana msichana huyo na kumuita mwizi, baada ya mkewe kurejea nyumbani ghafla.
Bwana huyo, Kevin Gaylor wa Colorado Springs Marekani, alikutana na msichana kwenye mtandao wa Craiglist.com na kumwambia aende kumtembelea nyumbani kwake. Hata hivyo mke wa bwana Kevin alirudi nyumbani ghafla, na kumfaya bwana huyo kupagawa asijue la kufanya.
Muda mfupi baada ya mke wake kuwasili, msichana aliyealikwa naye akafika. Kujaribu kuokoa jahazi bwana huyo alipiga simu polisi na kusema kuna mwizi nyumbani kwake. Gazeti la Metro limesema polisi watano walikwenda haraka nyumbani kwa bwana Kevin kupambana na mwizi ambaye waliambiwa alikuwa na silaha.
Badala yake polisi walikuta msichana mwenye umri wa miaka 20 akiwa nje ya nyumba ya bwana Kevin. Msichana huyo aliwaambia Polisi kuwa alisafiri kwa muda wa zaidi ya saa moja ili kukutana na Kevin, na kuwa walikuwa wakiwasiliana kwa muda wa wiki mbili kupitia simu na internet. Polisi walipogonga mlango wa bwana Kevin, alitoka na kuanza kuzungumza kwa sauti ya chini na kuwasihi polisi wamuondoe msichana huyo. Hata hivyo bwana huyo alikamatwa na kushtakiwa kwa kosa la kutoa taarifa za uongo kwa polisi.

Wezi waacha 'ushahidi' muhimu


Polisi nchini Sweden wamewakamata wezi wawili baada ya wezi hao kuacha haja kubwa karibu na mahala walipofanya wizi wao. Wezi hao walijisaidia nje ya nyumba moja katika eneo la Vara, katikati ya Sweden, muda mfupi kabla ya kuvunja nyumba na kufanya wizi.
Gazeti la huko limesema baada ya kuvunja nyumba hiyo walimkamata mwenye nyumba hiyo na kumfunga na kamba na kisha kujichukulia walichokuwa wakikitaka. Taarifa zinasema wezi hao waliiba fedha taslimu kronor elfu kumi, sawa na dola elfu moja na mia tano, pamoja na vifaa vingine na gari.
Mbali na kuhakikisha wanateketeza kila ushahidi ili wsikamatwe, walisahau kufukia kinyesi chao. Makachero katika upekuzi wao walikuta kinyesi hicho na waliweza kutumia teknolojia ya DNA na kuwatambua wezi hao. Mtandao wa habari wa Sweden umesema wezi hao waliweza kutambuliwa na hatimaye kukamatwa.

Bwana harusi mzee duniani

Bwana mmoja nchini India Hazil Abdul Noor, mwenye umri wa miaka mia moja na ishirini, ameweka historia wiki iliyopita, baada ya kufunga ndoa na mwanamke nusu ya umri wake.
Gazeti la Times of India limesema bwana huyo ambaye ni mjane, alifunga pingu za maisha na Samoi Bibi mwenye umri wa miaka sitini. Zaidi ya wageni mia tano walihudhuria harusi hiyo iliyofanyika katika kijiji cha Satgori, kilichopo kwenye jimbo la Assam.
Wageni zaidi ya mia moja walitoka upande wa bwana harusi, wakiwa ni pamoja na wanae wawili wa kiume, wanne wa kike, na watoto wao, na watoto wao, na watoto wao. "Haikuwa rahisi kumtafutia baba yetu mke" amesema mtoto wa kiume wa bwana harusi, akizungumza na gazeti la Times. "Hata hivyo kwa Kudra za Mungu, tumepata mama mpya, ingawa umri wake ni nusu ya wa baba yetu" amesema kijana huyo Hazi Azir. Bwana Noor anadhaniwa kuwa ndio bwana harusi mzee zaidi duniani.
Na Kwa taarifa yako........
Kwa wastani mwanamke huzungumza maneno elfu saba kwa siku, mwanaume huzungumza takriban maneno elfu mbili.....